1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LISBON: Pendekezo la kuregeza sheria ya kutoa mimba

11 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCTJ

Kura ya maoni inapigwa nchini Ureno hii leo,juu ya sheria kali za nchi hiyo kuhusika na kitendo cha kutoa mimba.Kura hiyo inahusika na pendekezo la serikali ya Ureno kuwa wanawake waruhusiwe kutoa mimba mpaka wiki 10 za mwanzo tu.Kwa hivi sasa,nchini humo wanawake wanaruhusiwa kutoa mimba ikiwa tu walibakwa,afya ya mzazi ipo hatarini au kama mimba changa ina kasoro fulani.