1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mahakama ya katiba Kongo yathibitisha ushindi wa Tshisekedi

Josephat Charo
10 Januari 2024

Mahakama ya katiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imethibitisha kuchaguliwa tena kwa rais Felix Tshisekedi baada ya kukataa mashauri mawili ya kisheria yaliyowasilishwa kuyapinga matokeo.

https://p.dw.com/p/4b5nF
DR Kongo | Mahakama (Picha ya ishara)
Mahakama imetulipia mbali shauri la kupinga kuchaguliwa kwa TshisekediPicha: Pond5/IMAGO

Mahakama ya katiba ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imethibitisha kuchaguliwa tena kwa rais Felix Tshisekedi baada ya kukataa mashauri mawili ya kisheria yaliyowasilishwa kuyapinga matokeo yaliyozozaniwa ya uchaguzi wa mwezi uliopita.

Mahakama hiyo imemtangaza rasmi Tshisekedi kama mshindi wa uchaguzi huo. Uamuzi huo wa mahakama unamfungulia mlango Tshisekedi kuhudumu kwa awamu nyingine ya miaka mitano katika taifa hilo la pili kwa ukubwa barani Afrika.

Soma pia: Umoja wa Mataifa waonya kukithiri kwa matamshi ya chuki DRC

Mahakama ya katiba imethibitisha ushindi wa Tshisekedi licha ya ripoti za waangalizi huru wa uchaguzi kudai kulikuwa na mapungufu wakati na baada ya uchaguzi wa mwezi Desemba mwaka uliopita ambayo yaliwafanya wagombea wa upinzani kutaka uchaguzi urudiwe na kudai kulitokea wizi.