1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mawaziri wa mambo ya kigeni EU wajadili kuhusu amani Libya

Sekione Kitojo
20 Januari 2020

Mawaziri wa mambo ya kigeni wa Umoja wa Ulaya wamekutana leo kujadili jukumu la kundi la mataifa hayo katika utekelezaji wa  mchakato wa amani ya Libya,ambapo wengi wanapendelea  kuazisha upya ujumbe wa jeshi la majini. 

https://p.dw.com/p/3WULQ
Josep Borrell, Aussenminister der EU
Picha: EU/F. Marvaux

Hali  hiyio imejitokeza  baada  ya  wahamiaji  wengi  kuingia  katika  mataifa  ya  Umoja  wa  Ulaya  na  kusababisha   na  ujumbe  huo ulisitishwa  mwaka  jana  wakati  ulipozuka  mjadala mkali  wa  wahamiaji.

Brüssel | Josep Borrell, Hoher Vertreter der EU für Außen- und Sicherheitspolitik
Mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep BorrellPicha: Reuters/F. Lenoir

Mazungumzo  hayo  mjini  Brussels yanakuja  masaa  kadhaa  baada ya  mkutano  kuhusu  Libya  mjini  Berlin  ambamo  viongozi  wa kimataifa  wameahidi  kuimarisha  vikwazo  vya  silaha  vya  Umoja wa  Mataifa  na  kufikisha  mwisho  usaidizi  wa  kijeshi  kwa makundi  ya  nchi  hiyo  yanayopigana.

Waziri  mkuu  wa  nchi  hiyo  anayekabiliwa  na  matatizo  Fayez  al-Serraj  anaungwa  mkono  na  Umoja  wa  mataifa  pamoja  na uwepo  wa  majeshi  ya  Uturuki, wakati  kamanda  hasimu  wake Khalifa  Haftar  anaungwa  mkono  na  Misri, Umoja  wa  Falme  za Kiarabu  na  Urusi.

Libya  imekuwa  katika  machafuko  tangu  kuondolewa  madarakani mwaka  2011  kwa  kiongozi  wa  muda  mrefu Moamar Gaddafi  na imekuwa  uwanja wa    mapambano  kwa  majeshi  hasimu  ya mataifa  ya  kigeni. Suala  hilo  linaonekana  kuwa  muhimu  katika usalama  wa  Umoja  wa  Ulaya, baada  ya  nchi  hiyo  ya  Afrika kaskazini  kuwa  lango  kuu  la  wahamiaji  wanaojaribu  kufika barani  Ulaya.

Katika  mkutano  wa  jana  Jumapili , Umoja  wa  Ulaya  uliahidi kusaidia  kutekeleza  makubaliano  yaliyofikiwa , ikiwa  ni  pamoja  na uwezekano  wa  kutuma  vikosi  vya  jeshi  chini  ya  bendera  ya Umoja  wa  Ulaya.

Brüssel Treffen Außenminister Deutschland, Frankreich, Italien & Großbritannien
Mkutano wa mawaziri wa mambo ya kigeni mjini Brussels , mawaziri wa Ufaransa, Ujerumani na Italia wakijadili kuhusu LibyaPicha: Reuters/F. Seco

Doria ya Sophia

Mataifa  wanachama  ambao  hawajawahi  kukubaliana  juu  ya  njia ya  kupiga  hatua  kuhusu  Libya, wanapaswa  sasa  kuamua  njia bora  ya  kuchangia  wanajeshi  watakaotumika  kuangalia makubaliano  ya  kusitisha  mapigano  na  kuheshimiwa  kwa vikwazo  vya  silaha.

Hii  inaweza  kujumuisha  kuanzishwa  upya  kwa  doria  za  jeshi  la majini  katika  bahari  ya  Mediterania  chini  ya  operesheni iliyojulikana  kama Sophia, ikiwa  kimsingi  ni  ujumbe  wa  Umoja  wa Ulaya  wenye  lengo  la  kuzuwia  usafirishaji  haramu  wa  binadamu na  kulinda utekelezaji  wa  vikwazo  vya  silaha dhidi  ya  Libya.

Mkuu wa sera za  mambo  ya  kigeni wa Umoja  wa  Ulaya  Josep Borrell  amesema  kabla  ya  mazungumzo  ya  leo  kuwa, kusitisha mapigano  kunahitaji uangalizi:

"Kuna uwezekano aina kadhaa ya kadhaa , lakini  usitishaji mapigano unahitaji  uangalizi. Huwezi  kusema, haya  ni  makubaliano  ya kusitisha  mapigano  na  baadaye unayasahau. Kuna  udhibiti  wa silaha, na udhibiti wa  vikwazo  vya  silaha. Kuna  aina  nyingi  ya uwezekano,  na  mawaziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Umoja  wa Ulaya  wanapaswa  kuamua cha  kufanya  ili kusaidia  utekelezaji  wa makubaliano  ya  mkutano  wa  jana wa  Berlin kuhusu  Libya."

Deutschland Libyen-Konferenz in Berlin
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Heiko MaasPicha: Reuters/A. Schmidt

Jana waziri wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ujerumani Heiko Maas ameelezea  hali  mbaya  yanayokumbana  nayo  wahamiaji  katika makambi  nchini  Libya. Siwezi  kusema  kuwa  naiangalia  hali ya wahamiaji  kuwa  kinyume  na  ubinadamu, na  kisha  nikubaliane kuwa  watu  warejeshwe huko. Tunapaswa  kuzungumza  tena  juu ya   operesheni Sophia  bila  shaka,"  aliiambia  televisheni  ya  taifa ARD. Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Italia  Luigi Di Maio amesema  jana  kuwa  Italia  iko  tayari  kuchukua  jukumu  la  mbele katika  kuangalia amani  nchini  Libya.