1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSomalia

Somalia: Wanajeshi walioko Eritrea kurejea nyumbani Disemba

Amina Mjahid
20 Desemba 2022

Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud amesema wanajeshi wanaopata mafunzo Eritrea wataanza kurejea nyumbani mwezi huu katika zoezi linalotarajiwa kuendelea hadi mwezi Januari mwaka 2023.

https://p.dw.com/p/4LDF3
Somalia Präsident Hassan Sheikh Mohamud
Picha: Farah Abdi Warsameh/AP/picture alliance

Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na raia wa Somalia wanaoishi Marekani wakati wa ziara yake nchini humo. Kwa miezi kadhaa, uvumi ulienea Somalia kwamba wanajeshi hao huenda wakapelekwa katika eneo linalokabiliwa na vita la Tigray, nchini Ethiopia.

Mohamud ambaye aliahidi kuwarejesha nyumbani wanajeshi wakati wa kampeni yake, aliwatembelea katika kambi za mafunzo nchini Eritrea, mwezi Julai.

soma zaidi:Hoteli iliyoshambuliwa na Al Shabaab yadhibitiwa Somalia

Mwezi Juni, mwaka uliopita, mtaalamu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na haki za binadaamu nchini Eritrea, Mohamed Abdelsalam Babiker, alizungumzia taarifa kwamba wanajeshi wa Somalia waliondolewa katika kambi za mafunzo ya kijeshi nchini Eritrea na kupelekwa kwenye uwanja wa vita huko Tigray, ambako waliongozana na wanajeshi wa Eritrea ambao wanaviunga mkono vikosi vya shirikisho vya Ethiopia kupambana na waasi.