1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchaguzi mkuu wafanywa nchini Zimbabwe

P.Martin29 Machi 2008

Uchaguzi wa rais,bunge na serikali za mitaa unaendelea nchini Zimbabwe.Wapiga kura walianza kupangana mstarini tangu alfajiri,hata kabla ya vituo vya kupigia kura kupata kufunguliwa.

https://p.dw.com/p/DX9A
***Kein Ende? - Seit 1980 steht Robert Mugabe erst als Regierungschef, dann als Präsident Simbabwe vor, Scholz*** Zimbabwean President Robert Mugabe greets supporters during an election rally at Qwanzura Stadium in Harare, Zimbabwe, 28 March 2008. President Robert Mugabe is seeking a further five-year presidential term and faces a major challenge from opposition Movement for Democratic Change (MDC) leader Morgan Tsvangirai and former finance minister, Simba Makoni, who is standing as an independent candidate after being expelled from the ruling Zanu-PF party. EPA/TAURAI MADUNA +++(c) dpa - Report+++
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe akiwasalimu wafuasi wake katika mkutano wa hadhara mjini Harare.Picha: picture-alliance/ dpa

Kiasi ya Wazimbabwe milioni 6 wameandikishwa kupiga kura,huku Rais Robert Mugabe akikabiliwa na kile kinachosemekana kuwa ni changamoto kali kabisa tangu kiongozi huyo kushika madaraka miaka 28 iliyopita.

Mugabe anapambana na kiongozi wa chama kikuu cha upinzani cha MDC,Morgan Tsvangirai na vile vile waziri wake wa zamani wa fedha,Simba Makoni alieondoka chama tawala cha Mugabe ZANU-PF.Viongozi hao wa upinzani wamelalamika kuwa Mugabe ana njama ya kufanya udanganyifu wa kura.Tsvangirai amesema,chama chake kimepata ushahidi wa udanganyifu mkubwa wa kura ikiwa ni pamoja na majina ya kubuniwa katika orodha ya wapiga kura,kaskazini mwa Zimbabwe.Mugabe amepinga tuhuma hizo.

Wazimbabwe wengi wanalalamika kuhusu hali mbaya ya uchumi wa nchi hiyo,ambayo hapo zamani ilikuwa na uwezo wa kulisha mataifa mengine barani Afrika.Hivi sasa,Wazimbabwe wanapambana na mfumuko wa bei uliopindukia asilimia 1000 na idadi ya watu wasio na ajira ni zaidi ya asilimia 80

Vituo vya kupigia kura vinatazamiwa kufungwa saa moja usiku.Matokeo ya mwanzo ya uchaguzi hayatarajiwi kabla ya Jumapili na itachukua siku kadhaa kuhesabu kura zote zilizopigwa.Zimbabwe imewapiga marufuku wasimamizi wa uchaguzi kutoka nchi za Magharibi.

Hakuna ripoti za machafuko makubwa,lakini polisi imesema, nyumba ya mgombea ubunge wa chama tawala,Judith Mkwanda imeshambuliwa kwa bomu la petroli katika mji wa kusini wa Bulawayo.