1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Umoja wa Ulaya waondoa vikwazo vya vyakula vya Japan

Zainab Aziz
13 Julai 2023

Umoja wa Ulaya umekubali kuondoa vikwazo vilivyokuwa vimebakia dhidi ya kuagiza vyakula kutoka Japan vilivyohusishwa na ajali iliyotukia kwenye kinu cha nyuklia cha Fukushima mnamo mwaka 2011.

https://p.dw.com/p/4Trbk
Japan l Nach dem Atomunfall im Kernkraftwerk Fukushima Daiichi
Picha: Air Photo Service/Handout/dpa/picture alliance

Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Ulaya, Ursula Von der Leyen, amefahamisha hayo leo mjini Brussels.

Katika taarifa yake Umoja wa Ulaya umesema kuondolewa vikwazo hiyvo kunatokana na matokeo chanya ya udhibiti uliuofanywa na idara za Japan kwenye vyakula hivyo.

Soma zaidi: Japan: Kesi ya uvujaji wa data yazua wasiwasi kuhusu wanasayansi wa kigeni

Vikwazo hivyo viliwekwa tangu kuharibiwa kinu cha nyukulia  cha Fukushima kutokana na tetemeko la ardhi pamoja na mawimbi ya Tsunami.

Licha ya kuondolewa vikwazo hivyo Umoja wa Ulaya utaendelea kuvikagua vyakula vinavoagizwa kutoka Japan kuhakikisha vina kiwango cha mionzi kinachoruhusiwa.