1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN: Kuzama baharini ndio chanzo kikuu cha vifo vya wahamiaji

26 Machi 2024

Shirika la Umoja wa mataifa linalohusika na Uhamiaji IOM, limesema kuzama ndio kimekuwa chanzo kikuu cha vifo vya wahamiaji katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.

https://p.dw.com/p/4e9Cr
Shirika la IOM lasema kuzama baharini ndio chanzo kikuu cha vifo vya wahamiaji
Shirika la IOM lasema kuzama baharini ndio chanzo kikuu cha vifo vya wahamiaji Picha: Simone Boccaccio/SOPA/IMAGO

Shirika la IOM inasema idadi ya waliozama baharini imepindukia 36,000. Shirika hilo la Umoja wa Mataifa linasema kati ya vifo 64,000 vya wahamiaji vilivyorekodiwa katika mwongo mmoja uliopita, karibu asilimia 60 vilihusishwa na kuzama. Kati ya vifo hivyo vya baharini, 27,000 vilitokea katika Bahari ya Mediterenia, njia ambayo imekuwa ikitumiwa na wahamiaji wengi wanaojaribu kufika kusini mwa Ulaya kutoka kaskazini mwa Afrika.

IOM lakini limesisitiza kwamba idadi hiyo iliyochapishwa katika ripoti hiyo haijakamilika.