1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urafiki na ushirika wa kinadharia baina ya SPD ya Ujerumani na CCM ya Tanzania

Othman, Miraji29 Septemba 2008

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM-Tanzania ziarani Ujerumani

https://p.dw.com/p/FR0v
Jengo la makao makuu ya Wakfu wa Friedrich Ebert mjini BerlinPicha: picture-alliance/ ZB

Chama cha Social Democratic, SPD, cha hapa Ujerumani , na kile cha Mapinduzi, CCM, huko Tanzania ni vyama vya kirafiki vilivyo na ushirika wa miaka tangu ya sabini wakati wa viongozi wa vyama hivyo, Willy Brandt na Mwalimu Julius Nyerere. Kwa wiki moja iliopita alikuweko ziarani hapa Ujerumani katibu wa itikadi na uenezi wa chama cha CCM, John Zephania Chiligati, ambaye pia ni waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makaazi, kwa mwaliko wa Wakfu wa Friedrich Ebert wa chama cha SPD. Mgeni huyo wa kutoka Tanzania alitembelea jengo letu la Deutsche Welle, na Othman Miraji alifanya naye mahojiano. Kwanza waziri Chiligati alielezea vitu gani vinavowaunganisha wana CCM na Wa-Social Democratic...